MACHOZI YANATIRIRIKA OOOOOOOH!!! LISSA UMENIUA?

Inashangaza Sio? Yawezekana Nikaonekana Chizi, Yawezekana Nikaonekana Sijitambui, Yawezekana Nakosa Mwelekeo.
.
Ndio, Yawezekana Ni Kichaa. Oooooh!!! Historia Ya Maisha Ya Vijana Wengi Imebebwa Na Wimbo Huu. Yawezekana Ikakushangaza!! Yawezekana Ikakuduwaza, Huu Ndo Ukweli Halisi Wa Maisha Ya Wanachuo, Vijana Wengi Wameguswa Na Wimbo Huu.
.
Ile Safari Ya “Kuamini Usipoaminiwa” Ile Safari Ya Kumsave “Love Of My Life” Ile Safari Ya “Mbona Hii Namba Ina Jina La Kiume” Ni Safari Halisi Ya Mapenzi Na Mahusiano Ya Vijana Wengi.
.
Uaminifu Kwa Vijana Unaonekana Ni Kiza Kizito Kwenye Nyanja Zote Za Maisha, Ofisini, Uchumi, Kisiasa na Kijamii. Ndio Ni Kiza Kizito Kutokana Na Changamoto Nyingi Wanazokutana Nazo Vijana Katika Ukuaji Wa Kuelekea Kutimiza Ndoto Za Maisha. Wamebeba “VIDONDA” Vizito Mioyoni Mwao.
.
Vidonda Vya Mateso, Uchungu, Vilio Vinatisha. Inashangaza Sio? Huo Ndo Uhalisia Wenyewe.
.
MAUMIVU HUWA MAKALI UKIMPA KITU UMPENDAYE NAYE AKAMPA AMPENDAYE” Ndio, Maumivu Yake Hayamithiriki, Hayaelezeki, Hayabebeki Na Hayasimuliki .
Oooh!!! DUNIA YA LEO, Hamna mtu anaependa kuwa Single. Kuwa single sio kwamba mtu hujui kupenda. Sababu kubwa ni kuchoka kujitoa kwa mtu halafu mwishoni unapata maumivu.
.
Inachosha kuamini na kumpenda sana mtu na mwishoe inaishia kusalitiwa na kuumizwa moyo.
.
Inachosha na inaumiza sana kujali, kuheshimu na kuonesha uaminifu lakini unaambulia kudanganywa na kupigwa danadana !
.
Inachosha kuwa na mipango mingi ya mbali na mtu ambaye lengo lake ni la muda mfupi!
.
Hivyo, kabla hujamHukumu mtu, ukamwita majina mabaya na kumlaumu katika msimamo wake wa maisha, hebu fikiria kwanza ni nini kimemfanya awe hivyo.
.
Vaa viatu vyao na uone maumivu waliyopitia. Wamepitia mengi ya kuumiza na kukatisha tamaa katika mahusiano. Hofu hiyo bado imewajaa mioyoni mwao. Hawana uhakika na yupi atakayefaa kupewa tena nafasi mioyoni mwao.
.
Ndio, wanayo mapenzi ya dhati, lakini uhakika wa nani apewe ndio haupo. Kama mtu akikupenda, jaribu kumuelewa, jaribu kumjali, jaribu kumuonesha kwamba, wewe sio kama wale wengine.
.
Ingia YouTube, Jifungie Chumbani Ukiwa Pekee Yako. Sikiliza Kwa Utulivu, Mwaga Chozi Uwezavyo, “TIRIRISHA CHOZI” Lia Kwelikweli. 

Ukimaliza Futa Chozi, Simama, Acha “KUTIRIRISHA MACHOZI Jikaze, Endelea Na Harakati Za Maisha. Pongezi Kwa @majani187 Hakika Huu Ni Mziki Unaoishi Daima.