NYOTA ING`AAYO

Na, James Pius.

Wahenga wanasema “Mtembea bure si sawa na mkaa bure”  msemo huu wa wahenga naufananisha na harakati mbalimbali za wasanii wa bongo katika kuteka hisia za mashabiki mbalimbali kuanzia watoto mpaka wazee ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

Mziki wa bongo maarufu kama Bongo fleva haijafahamika rasmi mpaka leo nani ni muanzilishi wake japo kuna watu mbalimbali ambao inasemekana ndio waanzilishi rasmi wa mziki huu kama Mike Mhagama mnamo mwaka 1996 ambaye alikuwa akijaribu kutofautisha mziki wa R&B na HIPHOP wa marekani  katika kipindi cha Dj show kilichokuwa maarufu kwa kipindi kile.
Leo sitajikita katika historia ya bongo fleva bali nimetua nanga yangu katika harakati za wasanii mbalimbali katika kuteka hisia za mashabiki kuanzia bongo mpaka mamtoni katika tambo zote kama Hiphop, R&b mpaka Afro pop na mziki unaotamba kwa sasa maarufu kama singeli.

Nyota mbalimbali za wasanii zilianza kung`aa tangu zamani katika ramani ya mziki ndani na nje ya mipaka ya Tanzania . Kuna makundi yaliyong`aa katika ulimwengu huu wa bongo fleva kama Kwanza Unit 1993 kundi lililotamba sana na mmoja wa wananchama ni Professa Jay, hata hivyo kuna makundi mengine mengi kama East cost team, TMK wanaume, TMK Family.
Lady Jay Dee maarufu kama komandoo  ni nyota ya kwanza kung`aa kwa upande wa wasanii wakike, alitoa album kama Machozi 2000 na ameshashinda tuzo mbalimbali kama video bora ya msanii wa kike channel O 2005 na best collaboration video (makini) with titi kutoka Uganda, 2003 channel O music video awards, video of the year( machozi) na tuzo mbalimbali za Kilimanjaro Music Awards na hivyo kuwa nyota ya kwanza kung`aa kwa upande wa anga za kimataifa hasa Africa.
Image result for LADY JAYDEE

Juma Kassim Ally Hii ni nyota nyingine iliyoanza kung`aa katika anga za kimataifa. Ana majina mengi maarufu kama Sir Nature, kiroboto, kibla, msitu wa vina mwenye album kama nini chanzo 2001 ugali 2003 ubinadamu kazi 2005 zote history 2006 ameshashinda tuzo mbalimbali za kimataifa kama tuzo za channnel O kama wimbo bora wa Afrika mashariki – Mugambo 2007 na tuzo za kutosha za Kilimanjaro Music Awards.
Image result for JUMA NATURE

Ambwene Allen Yessayah maarufu kama A.Y ni moja ya nyota iliyoanza kung`aa  mapema zaidi katika soko la Hiphop biashara na kufanikiwa kujitwalia tuzo ya Best video from Tanzania 2007, Kisima Music awards na wimbo wake wa usijaribu 2008 pearl of Africa music awards best Tanzanian male artist , channel O music video awards as Best East African video na tuzo kibao za Kilimanjaro Music Awards.
Image result for AMBWENE  AY

Kwa leo hizi ni nyota kadhaa zilizoanza kung`aa katika anga za kimataifa na kujitwalia tuzo mbalimbali.
Makala hii maalumu ya NYOTA ING`AAYO itakujia kila wiki hapahapa MALIQUIDHITZ hasa ikikuangazia wasanii wakali kutoka Tanzania waliofanya na wanaofanya vizuri nje ya mipaka ya Tanzania.